SciDev.Net

Pages

Sunday, August 9, 2015

Mratibu Mkaazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania alonga na Wanahabari wa Zanzibar




Na A.H.Hamad
Mratibu Mkaazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Alvaro Rodriguez amesema afisi yake inafanya kazi kwa karibu sana na mamlaka za serikali na taasisi za kiraia kuhakikisha kuwa Uchaguzi mkuu ujao unafanyika kwa umakini, uwazi na kwa amani.

Akijibu masuali ya waandishi wa habari katika mkutano na Wanahabari wa Zanzibar uliafanyika katika ukumbi wa afisi ndogo ya UN Zanzibar Bw. Rodriguez amesema ijapokuwa UN haina nguvu za kutosha kuhakikisha kuwa kila kitu kinaenda sawa lakini inafahamu kuwa inalojukumu la kuhakikisha kuwa inashirikiana na vyombo husika ili kupunguza joto la uchaguzi na kuhakikisha haki za watu wote zikiwemo za watoto, wanawake na walemavu zinaheshimiwa na kulindwa kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

Ametaja baadhi ya hatua zinazochukuliwa na UN katika kufanikisha hilo kuwa ni pamoja na utekelezaji wa Mradi wa miaka mitatu wa  Ujengaji Uwezo wa Demokrasia (Democratic Empowerment Project) ambao pamoja na mambo mengine unasaidia kuimarisha uwezo wa Tume ya uchaguzi Zanzibar na wadau mbali mbali wa uchaguzi wa uchaguzi ili dhamira ya kuhakikisha Amani iliopo inaendelea kudumu inafanikiwa.

Hata hivyo mratibu huyo mkaazi aliwakumbusha wanahabari kuwa pamoja na machango huo wa UN wanahabari nao wanajukumu kubwa la kuhakikisha uchaguzi wa Amani hasa kwa kuzingatia ushawishi wa yale wanayoyaandika, kuyatangaza na kuyapiga picha kwa wananchi wanaowafuatilia.” Himizeni Amani, toeni habari sahihi na shawishini mijadala/mazungumzo miongononi mwa wadau mtakuwa mmesaidia” alisema.

Akitoa ufafanuzi wa mchango wa Umoja wa Mataifa katika mradi huo wa ujengaji uwezo wa Demokrasia Msimamizi wa Mradi Bi Hamida Kibwana amesema Umoja wa Mataifa umeisaidia tume ya Uchaguzi kupata vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi na kuwakutanisha wadau wa uchaguzi na vijana katika majadala ya kisiasa ili kujenga mazingirira ya kuelewana na kukuaminiana kabla wakati na baada ya uchagu.

Sambamba na hayo mradi utajumuisha pia mafunzo kwa wanahabari ili waweze kuandika vyema habari za uchaguzi na kuwapatia pia mafunzo maafisa wa polisi juu ya njia bora ya kukabiliana na rabsha za uchaguzi bila kutumia nguvu nyingi na kwa njia ambayo inaheshimu haki za binaadamu.
Amesema mradi huo umesaidi pia kutayarisha maadili ya uchaguzi kwa Vyama vya siasa ambayo yalitiwa saini hivi karibuni Zanzibar na tayari maafisa wake wamepata fursa ya kujifunza utaratibu uliotumiwa na Kenya katika kuratibu matokeo ya uchaguzi ili yasilete mkanganyiko kwa wananchi na kuwa chanzo cha vurugu.

Nae Mkuu wa Afisi ndogo ya Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga amesema  Umoja wa mataifa unania ya dhati ya kuimarisha demokrasia Zanzibar na ndio maana pamoja na misaada mbali mbali inayotolewa katika kuhakikisha uchaguzi wa Amani imekuwa pia ikisaidia kuimarisha ushiriki wa wagombea wanawake katika uchaguzi  kwa kuwajenga uwezo wa kujinadi, kujiamini, na kushindana ili kupunguza pengo la usawa liliopo sasa katika vyombo vya kutunga sharia.

Mapema Mratibu Mkaazi wa umoja wa Mtaifa tananzia alilitaja tatizo la mabadiliko ya Tabia nchi na Nishati kuwa ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili Zanzibar ambazo Umoja huo umeamua kushirikiana na Serikali na taasisi zisizo  za kiserikali kuyapatia ufumbuzi kwa haraka kadri inavyowezekana.

No comments: