Sunday, June 17, 2012

GHANA AND ZANZIBAR HAVE ONE LINK IN COMMON


By Ali Haji Hamad, Pemba
Have you ever think that Zanzibar and Ghana have something  in common. Probable not - At a quick glance you may only notice differences . For example when you think of neighbouring sea Zanzibar is surrounded by Indian ocean but Ghana is neighbouring Pacific Ocean. In Zanzibar we export cloves but they export Cocoa. We are located at the Eastern part of  African Continent but Ghana is at the Western side. Nevertheless the truth is -we have something in common or let me say we are linked with at least  one historical thread. Pay look at the below photo.

"I have no doubt that you have started thinking of Forodhani".

 Kweli si umeena Mizinga. Any  way this is a photo taken from CapeCoast of Ghana from a Palace which had special place for keeping slaves.
For those people who had a chance to study history in their secondary education might be aware that  some of the slaves were taken from Zanzibar to CapeTown- South Africa and then CapeCoast in Ghana before being taken to America and elsewhere in Europe. Writings in this history shows vividly how Zanzibar and Ghana colonial rulers and slave traders were close allies at that time because of the trade.

Because in Zanzibar we had people who remained here just because slave trade brought them here from there original places - why don't we think of the possibility of Zanzibaries who remained in Ghana because of the same circumstances. One of my friend told me that in CapeTown their is a Community of Zanzibaries who were left there since those days of Ukoloni. Hao ni mbali ya hawa wa Zanzibari wachakachuaji wa siku hizi wanaozamia.
see more photos
Palace
Chumba cha wanaumeeee

Cape Coast Palace iliojumuisha pia "hifadhi" ya Utumwa

watalii wakisikiliza kwa makini na huzuni historia ya biashara ya utumwa

Adui alitarajiwa kutokea pwani na hivyo mizinga ilielekezwa huko

window to see
Nilikwisha sahau. Kumbe kuna minazi mingii na mizuri kama ya kwetuu vile hebu ona.


UTALII WA MISITU GHANA

Na Ali Haji Hamad, Pemba

Mapato katika Sekta ya Utalii hayaletwi na kuwa na vivutio vizuri na vingi pekee bali huletwa na ubunifu wa kuvifanya vivutio hivyo viwe vinavutia zaidi au hata visivyo vivutio basi vivutie. Hebu angalia ubunifu huu uliefanywa na Swahiba zetu wa Ghana katika msitu wao huu wa.KAKUM ulioko Kusini mwa Ghana.  Kimsingi huu msitu has nothing special to offer. Ni msitu tu kama ilivyo misitu yetu kama Ngezi au Msitu mkuu wa Micheweni .

"Bora hata Jonzani angalau kuna Vima Punju."
 Msitu wa KAKUM wenyewe una miti mirefu tu na Bonde moja liloko deep sana. Katika kuutembelea sikuwahi kuona hata karakaka sikwambii sikwambii nyoka au myama mwengine. Ila kwa ubunifu wao wameweza kuufanya msitu huu kuwa kivutio kikubwa kwa kutengeneza hiii hanging trail juu ya vilele vya miti. Ni mita kama mia saba hivi za kutembea katika hatari, woga na kiwewe lakini zinapokamilika kila mtalii anafurahi na kumuhadithia mwenzie. Ni hilo tu linalowafanya watalii wamiminike hukoo.
Sasa wa Zanzibar tunajitapa uchumi wetu unategemea utalii tumebuni nini la kuwavuta watu kutumia pesa zaidi.

Karibu KAKUM forest

Wageni wanaotembelea msitu wa KAKUM Ghana wakiwa katika hanging trail

Niliamua nami nijaribu japo kwa khofu kubwa 

Saturday, June 2, 2012

CLIMATE CHANGE AND COASTAL EROSION IN PEMBA ISLAND
By Ali Haji Hamad, Pemba.

To the world Climate change is almost a house hold terminology but not to the residents of Pemba Island, Zanzibar. Most of them do not understand its meaning, causes or impact. However the ignorance of these residents has not spared them from the effects of this calamity. The vivid effects is seen along the cost of the island whereby the rise of see water has affected the sea shores,  nearby rice farms and people residents.

Please watch the attached two minutes Video from the island.


Tanzania, Zambia zagaragazwa katika mechi za awali
Na Ali Haji Hamad
Pale kinaporoa kilemba ni muhali kwa mkuti kusalimika
Ndivyo wanavyoamini Waswahili wa Pwani. Usemi huu ulidhihirika leo katika mechi za kuwania kufuzu kucheza kumbe la Dunia huko Brazil mwaka 2014. Katika siku ambayo mabingwa wa Afrika Zambia imelala bao 2-0 mbele ya Waarabu wa Sudan kaika mechi ya kundi D, ilikuwa muhali kwa Tanzania nayo kustahimili wimbi hilo kubwa na hivyo yenyewe ikajikuta ikisalima amri mbele ya Ivory Coast kwa bao 2- 0 katika mechi ya kundi C huko Abidjan.  Ushindi huu ni mwanzo mbaya kwa timu hizi zote mbili ambazo zilionekana kupania kutaka kuvuka mabara kwenda Kusini mwa Amerika hapo 2014.

Timu nyengine zilizoanguka ni  Congo DR mbele ya Cameroon iliyochapwa 1-0 katika mechi za kundi H na Botswana mbele ya Afrika ya Kati iliyogaragazwa 2-0 kwenye mechi ya kundi A. Nyengine ni Guinea ya Ikweta iliyochapwa 3-1 na Tunisia  na Liberia iliyochakazwa kwa bao 3-1na Senegal katka mechi ya kundi J.
Sambamba na matokeo hayo kulikuwa na matokeo ya sare ya bila kufungana katika mchezo kati ya Kenya na Malawi   kundi F na Gambia na Morroco ziliotoka sare ya 1-1 katika mechi za kundi C. Bukinafaso na Congo nazo ziliishia suluhu ya 0-0 kundi E.

Tuesday, May 29, 2012

GOMBANI STADIUM - PEMBA ISLAND

Kama Ulaya Ulaya Vile
Who said that we are not ready for international matches. Just look at the renovated Gombani Stadium pitch. "Utaupenda". Are you thinking of buying it ! Sorry "hatuuzi'.

Sunday, May 20, 2012


MAKAAZI  HOLELA YA MILIMANI YANAVYOLITATIZA JIJI LA MWANZA.  (Makala hii niliichapisha kwa mara ya kwanza katika gazeti la nipe habari mwezi August 2011)

Na Ali Haji Hamad, Mwanza
  • ·         Yanaendelea kukua
  • ·         Kuyarasimisha haiwezekani
  • ·         Kuyaacha yalivyo yanatia kichefu chefu
  • ·         Huduma za usafi wa maji taka na taka ngumu zinakwama
  • ·         Hakuna bajeti iliyotengwa kushughulikia


Si siri kwamba Mwanza ni miongoni mwa majiji yanayokuwa kwa kasi nchini Tanzania Ukuaji huo unaonekana takriban katika Nyanja zote zikiwemo zile za kiuchumi na kijamii. Wanaotembelea Mwanza watakuwa ni mashahidi wa ongezeko la ukuaji katika biashara za magari, mabenki, mahoteli, na biashara za kati na kati za maduka. Aidha ongezeko la Idadi ya watu nalo ni dhahiri. Wingi wa watu huonekana sio tu kwa idadi kubwa ya wale wanaokwenda na kurudi katika mitaa ya jiji hilo bali pia katika utafutaji huduma kama vile za kiafya, ulipaji wa bili za maji na umeme na foleni ndefu katika mabenki. 

Takwimu nazo zinaonesha hivyo. Idadi ya watu Mwanza sasa inakisiwa kuwa 1,269,257 kutoka 1,200,000 mwaka 2010. Katika sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 idadi ilikuwa 476,646. Wakati huo ongezeko la kimaumbile lilikuwa asilimia 3.2 na kasi ya uhamiaji mijini ilikisiwa kuwa asilimia 8.


Ni faraja pia kwamba hata sura ya mji wenyewe nayo imebadilika. Kwa wale waliolipa kisogo jiji hili katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na kurejea tena hivi karibuni kama mimi, hawatakosa kuvutiwa na sura ya mabadiliko ambayo yamekuwa yakitokea. Barabara nzuri za katika kati ya jiji, magorofa mapya yaliyomalizika na yanayoendelea kujengwa, bustani nzuri katika baraba bara za Nyerere na  mzunguko (round about) wa samaki katika barabara ya Kenyata ni miongoni mwa mambo yanayolipa jiji hilo sura ya matumaini. 


Hata hivyo nyuma ya sura  hii ya matumaini ya jiji la Mwanza kuna sura mbaya na ya chukizo inayoweza kumfanya mtu asahau uzuri wote niliokuwa nimeudokeza hapo awali. Chukizo hili si jengine bali ni lile linalotokana na makaazi holela ya milimani. Makaazi haya yametapakaa tokea kandokando ya jiji hilo katika milima ya Mkolani, Mahina, na Kirumba hadi katikati ya jiji lenyewe katika milima ya Igogo, Seketure na Bugando. Kwa mujibu wa utafiti wa mabadiliko na mageuzi katika serikali za mitaa uliofanywa na Siri Lange wa taasisi ya Chr. Mischelsen kwa kushirikiana na taasisi ya Utafiti juu ya Umasikini ya Tanzanaia (REPOA) makaazi hayo holela yamo takriban katika vilima 14 vya mji huo.

Japo inaweza kuonekana kuwa makaazi holela si jambo geni kwa jiji kama Mwanza ambalo zaidi ya asilimia 70 (makaazi 49000) ya makaazi (65,500) ya jiji hilo hayakupimwa lakini hili la makaazi ya milimani lina uzito wa kipekee. Kwanza ni kutokana na nafasi (position) ya milima hiyo katika sura ya jiji la Mwanza. Kwa mfano milima ya Igogo ipo katikati mno ya Mwanza kiasi kwamba kuendelea kubakia katika sura yake hiyo itaendelea kuwa sawa na doa jeusi katika shati jeupe hata kama maeneo mengine ya mji yatapendezeshwa kiasi gani.



Pili makaazi ya milimani yanahitaji mtazamo wa kipekee kutokana na umuhimu wa maeneo hayo kwa mazingira na usafi wa jiji. Usafi wowote utakaofanywa katika mji wa Mwanza na kupuuza maeneo hayo itakuwa ni sawa na kuweka maji kwenye pakacha kwa sababu uchafu utakaopuuzwa milimani ni rahisi kushuka wenyewe ama kushushwa na mvua kuja maeneo ya chini na pengine kwenye ziwa ambalo ni chanzo kikuu cha maji yanayotumiwa majumbani katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kagera.
Tatu makaazi ya milimani yanahitaji mtazamo wa kipekee kutokana na kuwepo na hadithi za miaka mingi za kulishughulikia tatizo la makaazi holela ya huko ambazo hadi tunaandika makala hii hazijaleta mafanikio.

Hadithi za kutafuta suluhisho
Kwa uchache hadithi za kutafuta suluhisho la makaazi holela katika makaazi ya milimani ya  jiji la Mwanza lina miaka isiyopungua 12.  Zilianzia mwishoni mwa miaka ya 1998 wakati serikali ya Tanzania ilipoamua kupanua katika manispaa mradi uliokuwa umeanzia Dar es salaam wa Sustainable City Programme ikiwa ni sehemu ya miradi kadhaa ya aina hiyo chini ya Umoja wa Mataifa. Mwanza ikiwa manispaa wakati huo ilianzisha mpango wake uliojulikana kwa jina la Sustainable Mwanza Programme. Mradi huo baadaye ulibadilishwa jina na kuitwa Capacity Building for Environmental Management (CBEM) baada ya kupata ufadhili wa shirika la maendeleo la Denmark DANIDA wa dola za kimarekani 1.9 milioni ambazo ni takriban shilingi za Tanzania  bilioni tatu. Mradi huo ulioishia mwaka 2003 ulilenga kulijengea uwezo jiji la Mwanza wa kushughulikia mazingira ya jiji hilo ikiwemo mifumo ya maji taka, taka ngumu na kuboresha miundo mbinu ya kimazingira katika makaazi holela.  Kumbu kumbu pekee iliyoachwa na mradi huo kwa watu wa kawaida ni zile bara bara za miguu zilizojengwa katika wadi za Igogo na Pamba ambazo mwendelezo wake uliisha wakati mradi ulipoisha.

Kiongozi mmoja wa jumuiya ya kihabari iliyoshiriki kwa karibu wakati wa utekelezaji wa mradi huu aliniambia kuwa mpango ulikuwa ni pamoja na kuhamisha makaazi holela na kwa wkati huo yalikuwa ni 35000 na yalihitaji shilingi za Tanzania 50 bilioni. Sasa kwa mujibu wa takwimu za 2008 za jiji laMwanza kuna makaazi 65,500 na kulishughulikia tatizo lake inahitaji shilingi Billioni 200 kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe.

Wakati mradi wa CBEM ukiendelea mwezi April 2001 Shirika la Maendeleo la Denmark Danida lilizindua mradi mwingine uliojulikana kama Sustainable Development Programme in Mwanza uliokuwa na madhumuni matatu. Kwanza kuboresha mazingira ya makaazi holela kwa mujibu wa vigenzo vya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Makaazi UN-HABITAT. Pili ni kuzijengea uwezo CBOs na NGOs ziweze kusaidia kazi hiyo. Tatu ni kusaidia upatikanaji wa haki za kisheria za watu waishio katika makaazi holela ya milimani.

Kwa kuanzia mradi ulikuwa umezilenga kaya 2,500. Wananchi walishirikishwa katika kuchagua mahala pa kupitisha barabara na maeneo ambayo yangeweza kuanzishwa vituo vya afya na kujengwa shule. DANIDA kwa kushirikiana na  Chuo Kikuu cha Ardhi  na Upimaji (UCLAS) walikuwa na kazi ya kupima maeneo na kuetengeneza ramani ili kufahamu maeneo yatayotumika na nyumba ambazo zingestahiki kubomolewa. Wananchi walitakiwa kuchangia shilingi 20,000 kila kaya kusaidia zoezi  hilo kendelea na ili kuwafanya walione ni la kwao.

Hakuna hasa anaejua kilichotokea pale mwezi Agosti 2002 DANIDA walipotangaza kujitoa katika mradi huo na wakaondoa pia shilingi milioni 200 zilizokuwa zimetengwa kwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huo. Hivyo hadithi nyengine ya kutafuta suluhisho la makaazi holela nayo ikaishia patupu huku wale wanaolitakia mema jiji la Mwanza wakiwa hawajui kilichotokea. Inavyoonekana si wananchi wa kawaida tu ambao hawajui kwanini mipango ya kutafuta suluhisho kwa tatizo la makaazi holela ya milimani zinaishia kuwa hadithi za paukwa pakawa bali hata Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Josephat Manyerere. Nilipomuuliza kuhusu kinachokwamisha mipango mbali mbali ya kushughulikia tatizo la makaazi holela ya milimani katika jiji la Mwanza  alisema yeye hafahamu kuhusu uwepo wala utekelezaji wa mipango hiyo na anahitaji kufanya utafiti kwanza.
“Unajua sisi tumekuwepo madarakani kwa miezi minane tu na hatufahamu mambo hayo yaliyofanyika nyuma. Wewe mwandishi nenda tu sisi tutafanya utafiti tukiwa tayari tutakuita” aliniambia Meya huyo ambae pia ni diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Ni zaidi ya miaka 10 imepita tokea mradi wa kurkebisha makaazi ya Milimani ulipofeli na makazi ya milimani sio tu kwamba hayajaboreshwa bali pia yamekuwa yakiongezeka na kuifanya hali kuwa ngumu zaidi. Suala kubwa ambalo mtu anaweza kujiuliza kwa sasa jee ni ipi hali ya Makaazi ya milima na hatima yake  ni ipi? Je sasa ni ruksa au imeshindikana tu kushughulikiwa? Na ni wapi zilipoishia hadithi za kulishughulikia tatizo hili?

‘Ruksa’ kukaa Milimani Mwanza
Kwa viongozi wa jiji la Mwanza unapowauliza iwapo makaazi holela ya milimani sasa yamepata baraka, ama ni “ruksa” kuwepo, huwa wanapata kigugumizi kutowa jawabu la moja kwa moja lakini si kwa afisa maendeleo ya jamii wa mkoa wa mwanza, Isaac Ndasa. Bwana Ndasa yeye aliniambia mabadiliko ninayoyaona katika makaazi ya milimani Mwanza si ongezeko la makaazi bali ni dhana juu ya makaazi yenyewe.

“Dhana ya zamani ilikuwa kukaa milimani ni haramu lakini dhana ya sasa ni kwamba kukaa milimani si tatizo ikiwa mtu atafuata taratibu za huko” alisema afisa huyo na kuongeza kwamba inawezekana hiyo ndio sababu ya kuonekana kwamba makaazi ya huko yanakua.
Huu unaweza kutafsiriwa kwamba ni msimamo wa afisi yake lakini ushahidi unaonesha kuwa ni msimamo pia wa afisi za wengine wanaoogopa kusema wazi wazi kama vile afisi ya jiji la Mwanza..Kwa mfano mtu wa kawaida anapoona jitihada za kufikisha miundo mbinu ya umeme na maji huko japo kwa wateule wachache wenye uwezo katika wakati ambao watu walitarajia kuona mikakati ya kuhama au kuhamishwa ni ishara kwamba labda sasa makaazi hayo holela yameanza kupata baraka. Hata ule ukimya tu juu ya ujenzi wa makaazi mapya huko mengi yao yakiwa ya chumba kimoja au viwili nayo ni ishara nyingine kwamba labda sasa ni ruksa.


Kwa vyovyote itakavyokuwa watu wanaofuatilia tatizo hili la makaazi holela ya milima ya Mwanza akiwemo Mlagiri Kopoka wa Nyakato wanauchukulia  msimamo kwamba makaazi ya milima ni ruksa ulioelezwa na Afisa maendeleo jamii ywa mkoa wa Mwanza na ule usioelezwa wazi na jiji kuwa ni msimamo uliotokana na kukata tamaa au wa kujikosha baada ya ahadi kadhaa za kwamba tatizo hilo linashughulikiwa kuishia patupu. Kwa mfano, mbali na jaribio la kushughulikia tatizo la makaazi holela ya milimani nililolitaja hapo awali la mwaka 2001 ambalo halikufanikiwa kulikuwa na jaribio lingine pia mwaka 2002. Afisa wa Mipango miji ambae pia ni Mratibu wa mpango wa urasimishaji makaazi mwanza Maduhu Kazi, aliliambia gazeti hili kwamba katika mwaka huo manispaa ya Jiji La Mwanza ilitoa namba za nyumba kwa wakaazi wote wa huko ili kuwatambua lakini baadae hakuna kilichoendelea.

Mwaka 2005 jiji pia lilipiga picha za angani za makaazi yote ya milimani ili kupata picha halisi ya maeneo ya huko na baadae kufuatiwa na tamko la mkurugenzi wa jiji ya kuwataka wakaazi wa huko wahame na wahamie katika maeneo mengine lakini hakuna aliyehama.

Mwaka 2008 wakati naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dk. Asha Rose Migiro alipotembelea jiji la Mwanza na kuonana na Mkurugenzi wa jiji hilo Wilson Kabwe ambae ndie mkurugenzi wa sasa. Vyombo vya habari vilimkariri Mkurugenzi huyo akimueleza Dk. Migiro kwamba wameanza kuboresha maeneo ya milimani kwa kutengeneza michoro ya kuboresha makaazi hayo yakiwemo ya Mkolani na Kiloleni na akasema watakaohamishwa watapelekwa katika viwanja 5,000 vilivyokwisha pimwa kwa kazi hiyo.

Mkurugeni huyo hakuwahi kukanusha kauli hiyo hapo kabla hadi nilipomuuliza utekelezaji wa mpango huo hivi karibuni. Alisema yeye hakuwahi kutowa kauli hiyo na anachoweza kusema ni kwamba kuna viwanja 6,000 vimepimwa kwa ajili ya kuboresha makaazi Mwanza na si kwa watu wa milimani pekee. Nilipomuuliza maeneo vilipo viwanja hivyo aliniambia: 

“Si muhimu kujua viwanja viko maeneo gani wewe jua tu kwamba kuna viwanja 6,000 vimepimwa kuboresha makaazi” 

Afisa Mipango miji wa jiji la Mwanza Maduhu Kazi nae aliniambia kwa kadri anavyofahamu hakuna viwanja 5000 vilivyotengwa kwa ajili ya wakaazi wa milimani. Alisema jiji limekuwa katika harakati za kupima viwanja kwa ajili ya watu wote. Alifafanua kuwa katika utekelezaji wa hilo wao wanaendesha mradi unaojulikana kama mradi wa viwanja 3,500 na tayari wamefanikiwa kupima kupitia mradi huo jumla ya viwanja 1,700. Hata hivyo hakuna vyovyote katika viwanja hivyo vilivyokusuduwa watu wataohama au kuhamishwa kutoka makaazi holela ya Milimani. “Hivi ni viwanja kwa ajili ya kila mtu, si vya wakaazi wa milimani” alisisitiza afisa huyo.

Majaribio mengine ya hivi karibuni ambayo mtu angedhani ulikuwa ukombozi muafaka kwa makaazi holela ya Milimani ni mradi wa kupanga upya makaazi (urasimishaji) uliofadhiliwa na Wizara ya Ardhi na Mradi uliolenga kupata usaidizi wa UN-HABITAT kuboresha makaazi holela katika milima ya Mwanza.

Urasimishaji Makaazi
Kuhusu Mradi wa kurasimisha makaazi ambao umeanza tokea mwaka 2009 jiji la Mwanza lilipanga kurasimisha makaazi 15,000 na kusajili 45000 pamoja na kuyapatia hati kwa kipindi cha miaka miwili kupitia mradi huo wenye thamani ya shilingi 1.6 bilioni ambapo hadi sasa wamefanikiwa kurasimisha makaazi 10,333.

Afisa mipango wa jiji la Mwanza alisema hata hivyo urasimishaji huo ambao hufanywa kwa kutengeneza upya ramani za maeneo husika, kupima viwanja na kutoa hati na kuweka barabara za ndani ya mitaa hata hivyo hautoyahusisha maeneo ya milimani kwa vile yanakatazwa kwa mujibu wa sera ya mipango miji ya mwaka 2007 na sheria ya ardhi ya 1999.

Afisa huyo akitoa ufafanuzi alitaja sababu tatu ambazo zinapelekea maeneo ya milimani kuachwa katika mpango wa urasimishaji kwamba kwanza ni kutokana na  Sera ya mipango miji ya mwaka 2007 ambayo ndiyo iliyoandika utaratibu wa urasimishaji makaazi imekataza kurasimisha maeneo ya milimani, mabondeni na maeneo yaliyokwisha pimwa. Pili alisema urasimishwaji hautofanywa katika makaazi holela ya milimani kwa sababu zoezi hilo linaweza kupelekea kubomolewa kwa baadhi ya makaazi jambo ambalo ni kinyume na maelekezo ya mradi wenyewe. Na sababu ya tatu Maduhu alisema ni kutokana na ukweli kwamba ni vigumu katika maeneo ya milimani kupata ardhi inayokubalika kisheria kurasimisha.


Alisema wakati katika maeneo ya kawaida eneo la chini linalokubalika kurasimishwa ni mita za mraba 120 katika eneo la milimani kiasi cha mita za mraba 300 zinahitajika. Alisema hiyo ni kutokana na ukweli kwamba katika eneo la milimani panahitajika pia papatikane eneo la kupanda miti ili kuzuia mmong’onyoko na eneo la kutosha kuchimba makari ya maji machafu na vyoo.

Mradi ulioota Mbawa
Ama kuhusu mradi wa UN HABITAT huu ulikuwa ni mradi wa ushirikiano kati ya jiji la Mwanza na Shirika la Umoja wa mataifa linashoghulikia makaazi la UN HABITAT. Mradi huu ulilenga kuimarisha miundombinu katika mkaazi hayo ya milimani na kuwapatia fursa ya kuhama na kuhamia mahala pengine wale ambao wangependa kuhama. Hata hivyo licha ya Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe kukaririwa na vyombo vya habari akimueleza Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dk. Asha Rose Migiro mwaka 2008 kuwa andiko la Mradi lilikuwa tayari miaka mitatu baadae (hadi 2011) bado hakuna dalili zozote za kuwepo kwa mradi huo.
Nilipoomba ufafanuzi kuhusu mradi huo Mkurugenzi huyo alisema
 “Ile ( UN –HABITAT) ni taasisi ya kimataifa. Mchakato wake unachukua muda mrefu, wakiwa tayari wewe utaona”.
Kauli Hewa
Wakati ‘mishemishe’ hizo za kuwafanya wanaharakati wa mazingira, watetezi wa haki za binaadamu na wananchi kwa jumla waone kwamba kuna jitihada za kulishughulikia tatizo la makaazi holela ya milimani zikiibuka na kufifia miaka nenda miaka rudi imebainika kuwa sehemu kubwa ya kauli  zilizokuwa zikitolewa na Manispaa ya jiji la Mwanza zilikuwa ni kauli za midomoni zaidi kuliko za kitaalamu na mara nyingi zilitolewa kukidhi mahitaji ya wakati. Kwa mfano wakati jiji likizungumzia kuwahamisha watu na kuwapeleka mahala pengine halijawahi kutenga wala kupima viwanja kwa ajili ya kuwahamishia watu hao wala kuweka fedha katika bajeti kwa kufanikisha zoezi hilo.

Hapakuwahi kuwepo na bajeti ya jiji ya kulishughulikia tatizo hilo katika miaka iliyopita na hakuna bajeti ya kulishughulikia tatizo hili katika mwaka huu wa fedha 2011/2012 kwa mujibu wa Meya wa jiji la Mwanza Bwana Josephat Manyere na Mkurugenzi wa jiji Wilson Kabwe.


Matata Henry Matata Mwenyekiti wa kamati ya Mipango ya jiji la Mwanza ambae pia ni Diwani wa Kata ya Kitangiri (CHADEMA) yeye alisema tatizo la makaazi holela ya milimani ni kubwa na ni vigumu kushughulikiwa kwa bajeti ya jiji
 “Labda kama zipatikane serikali zenye pesa zao zisaidie”.

Mbali na kutokutengewa bajeti tatizo hilo pia halijaandaliwa mpango wowote wa uhakika wa muda mfupi, muda wakati au muda mrefu kulishughulikia hata katika wakati huu ambapo serikali ya Halmashauri ya jiji la Mwanza inaongozwa na Chama cha Upinzani cha CHADEMA. Nilipomuuliza Meya wa Jiji la Mwanza kwamba wao wakiwa ndio wanoshikilia usukani wanamipango gani kuhusiana na tatizo hilo alisema hawakuingia na mkakati wowote kuhusu makaazi holela ya milimani.

“Hili jambo si la mtu mmoja huwezi kuwa na mikakati juu ya jambo kama hili ni mpaka uwasikilize wenzio wanasemaje” 

Labda kukosekana huku kwa mipango ya dhati ya kulishughulikia tatizo hili kumetokana na ukweli kwamba bado uongozi wa juu wa jiji la mwanza haujakubali kwa dhati kwamba makaazi holela ya milimani ni tatizo.
Nilipomuuliza Mkurugenzi wa jiji Wilson Kabwe anaichukuliaje hali ya makaazi holela ya milimani alinijibu kwa kuniuliza suali pia: 

“Wewe umeona hizi ndio squatters?” “Haya ni makaazi tu. Hayajapangiliwa vyema basi” alisema na kuendelea kuhoji: “Wewe umewahi kuona squatters za wapi. Hebu nenda Kibera (Nairobi), nenda na Zaire (CapeTown) uone. Watu wanatembea zaidi ya kilomita moja huko kufuata vyoo vya maboksi vilivyowekwa barabarani” alisema

Alisema haoni kwamba hali ni mbaya katika makaazi hayo ya milimani kama watu wanavyopenda kusema. Alisema japo watu wana vyoo vibovu lakini wanavyo tofauti na sehemu nyengine na akasisitiza kwamba hali ni bora kuliko maeneo mengine.

Hata hivyo mama Mashaka mmoja wa wakaazi wa milimani katika milima ya Igogo alisema hajawahi kuwaona viongozi wa jiji wakitembea huko zaidi ya wale wanaokwenda mara moja kwa mwaka kudai kodi za viwanja za shilingi 10,000/=.

Maisha Milimani
Pamoja na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Wilson Kabwe kudhani kwamba  makaazi holela ya milimani Mwanza si tatizo sana kwa sababu tu hayajafikia viwango vya Kibera (Nairobi) na Zaire (CapeTown) hali ya maisha na huduma za kijamii milimani kwenyewe inaeleza tofauti.


Katika ziara ndefu ya kutemblea milima ya Mkolani Igogo, Bugando, Mkuyuni na Mahina nilishuhudia mambo kadhaa ya kuthibitisha adha na hali ya kukatisha tamaa ya huko. Mojawapo ya mambo hayo ni ulemavu wa mzee Hoza (57) mkaazi wa milima ya Igogo. Kwa mujibu wa maelezo ya mama Betty, mke wa Mzee Hoza, baba huyo amepata ulemavu wa kudumu baada ya kuvunjika mgongo alipoanguka wakati akitembea katika vigingi vya vichochoro vya huko kwenda mjini miezi sita iliyopita. Kwa sasa mzee Hoza hawezi kusimama wala kukaa. Baiskeli ya magurudumu matatu nilioishuhudia hapo mke wake aliniambia ilitafutwa imsaidie lakini haijamsaidia sana kwa sababu hapana mahala popote anapoweza kuiendesha baiskeli hiyo zaidi ya ndani ya boma la nyumba yao ambayo uwanja wake upana na urefu wake hauzidi mita 3. Mama Betty alinieleza kuwa kwa sasa kigari hicho hutumika tu kumtolea kitandani na kumpeleka ukumbini kuoga na kumrejesha kitandani.

Mama Betty alieleza kuwa hali ilikuwa ngumu zaidi katika siku za awali ambapo  Mzee Hoza mara kwa mara alikuwa akihitaji kupelekwa Hospitali ya Bugando. Anasema walikuwa wanalazimika kumbeba kwa mikono masafa marefu katika mahala ambapo hata vichochoro vya kupita naye navyo ni shida.
Ubovu wa njia hata za kutembea kwa miguu ambao ni chanzo cha ulemavu wa kudumu wa Mzee Hoza ni moja tu ya adha zinazowakumba wakazi wa Milimani.

Mambo mengine ambayo hayawezi kufichika hata kwa mtu atakayetembea siku moja tu katika makaazi Holela ya milimani ni kuzagaa kwa maji machafu yanayotirirka kutoka majumbani na makaro yaliyopasuka. Uchache na ubovu wa vyoo, kukosekana kwa mifumo ya kuhifadhi taka ngumu, ukosefu wa miundo mbinu ya maji taka, shida ya maji na nyumba chache tu zenye umeme. Hali ya kukuta karo ya choo pembeni ya dirisha la mtu mwingine au kibanda cha choo mbele ya nyumba ni ya kawaida.

Mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama Mashaka alituambia watu wa milimani sio tu kwamba wanategemea vyoo ambavyo ni vibovu na vyengine vimejaa lakini kuna kundi kubwa pia halina hata hivyo vyoo. Alituambia kundi hili hujisaidia kwenye mifuko ya plastiki na kutupa vinyesi hivyo mahala popote watapojaliwa.
“Hapo uliposimama hapo ndugu mtangazaji usingeweza kufika leo kama si kelele zangu ninazopiga kila siku. Hujisaidia kwenye mifuko na kutupa uchafu wao kila mahala mpaka hapa nyumbani kwangu” aliniambia mama mashaka.
Mama huyo aliendelea kueleza kuwa mbali na tafrani ya watu kuishi bila vyoo hata wale walionavyo nao wana tatizo kwamba vyoo vyao vinapojaa hawana jinsi ya kuvitapisha. Watu hawa husubiri mvua inaponyesha na kutiririsha uchafu wao  pamoja na maji ya mvua jambo ambalo alisema linatishia afya zao. Mama Mashaka alilaumu jiji la Mwanza kwamba wanachofanya ni kukusanya tu shilingi 10,000/= lakini hakuna huduma watowayo.

Tatizo la ugumu wa kusafisha maji taka lilizungumziwa pia na Msaidizi meneja uhusiano wa mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (MWAUWASA) Mwanza, Robert Masunya. Meneja huyo alisema hali mbovu ya ukosefu wa miundo mbinu ndio kikwazo kikubwa.

Alisema kwa hali ilivyo sasa hakuna njia yoyote ya kufikisha bomba la maji taka katika maeneo ya milima kama ya Igogo wala njia ya kufikisha gari la kufyonza maji taka.
“Kama gari linafika isingekuwa tatizo. Tuna magari ya kutosha hapa kwa ajili ya kazi hiyo" 
Masunya nae alilaumu pia uongozi wa jiji la Mwanza kwamba haujafanya jitihada za kutosha kurekebisha hali mbaya ya huko. Amesema hali hiyo inakuwa kikwazo kwa mipango ya MWAUWASA ya kudhibiti maji taka.

Pamoja na tatizo la maji taka wakaazi wa milimani wanakabiliwa pia na tatizo la kutupa taka ngumu. Katika ziara ya milimani iliyofanywa na mwandishi wa makala hii hakuwahi kushuhudia kontena lolote lililowekwa mahala kwa ajili ya kuhifadhi taka ngumu. Hata lile dogo lenye ukubwa wa ndoo ya plastiki ambalo lingeweza kuwekwa upenuni kwa nyumba halionekani popote.

Mama mashaka anasema wanapowauliza watu wa jiji kuhusu mahala pa kutupa taka ngumu huwaelekeza waende kutupa taka hizo katika kontena la sokoni. Kutoka milima ya Igogo anapoishi mama mashaka na Sokoni anakoelekezwa kutupa takataka ni umbali wa zaidi ya nusu kilomita.
“Hebu weye mtangazaji ona na miguu yangu hii mibovu halafu niende kutupa taka sokoni. Mi siwezi, natupa tu popote kama wanavyofanya wenzangu” alisema akionesha miguu yake aliyokua ameifunika kitenge.

Hali hii mbaya ya mazingira inazidisha tishio la milipuko kwa wakaazi wa milimani. Wakaazi wa huko akiwemo mama Mashaka analijua hilo. Yeye anadai jiji halitaki kuwasaidia ndio maana kila linapotokea tatizo wao ndio wa mwanzo huko kuathirika.
Hayo ni mbali ya ugumu wa kufikisha huduma muhimu za dharurua kama vile za zimamoto ama gari la kubebea wagonjwa pale linapotokea la kutokea.

Ikiwa wewe ni muumini pia wa haki za watoto na unadhani pia watoto wana haki ya kucheza, pengine wawe na kijiwanja kidogo hivi cha kucheza mpira au hata kufukuzana tu wenyewe na kufurahi basi haki hiyo haipatikani. Wenyewe hukaa tu juu ya majabali na kushangaa wale wageni wachache wanaofika huko ama kuangalia gari zipitazo barabarani na mara nyingine mitumbwi ieleayo ziwa Victoria.

Hata hivyo katikati ya adha hizi zinazowakumba wenyeji wa makaazi holela ya milimani bado kuna jambo moja zuri linalowafanya kutabasamu. Jambo hilo si jingine bali ni upendo na ujirani mwema miongoni mwao.
Bi Sophia John aliniambia kuwa watu wanaoishi milimani wanapendana sana kwa sababu kila mmoja anamuhitaji mwenziwe.
“Huku hata ukiwa na mgonjwa tu basi huwezi kumfikisha barabarani peke yako ni lazima upate msaada wa majirani. Hili linatufanya tuwe kitu kimoja” alisema Bi Sophia.

Hata hivyo pamoja na kuishi kwa upendo nilipowauliza kuhusu uwezekano wa kuhama na kuhamia mahala pengine wengi wao walionesha utayari wa kufanya hivyo. Mmoja wao ni mama Mama Betty amabae wamekaa huko yeye na mumewe na watoto wao kwa zaidi ya miaka 30 sasa.

Maisha ya huku ni tabu mno basi tu ndio tumezoea. Maji ndio hayo tunanunua na yanapokatika uende kufuata ziwani kule. Utapandisha ndoo ngapi huku?” alihoji mama huyo
Alisema alikwisha wahi kusikia kwamba watahamishwa na kupelekwa mahala pengine palipo bora zaidi lakini hajui mipango hiyo iliishia wapi na wao binafsi hawajawahi kuulizwa kuhusu hilo.

Sura zinazokinzana
Utayari wa wakaazi wa milimani wa kuhama makaazi yao ambayo wengine wameishi kwa zaidi ya miaka 30 kutokana na adha zilizoko unaweza kumfanya mtu kuvunjika moyo na apoteze hamu ya kuishi milimani.

Kama wewe ni mmoja wao ni kwa sababu tu haujawahi kutembelea kwenye milima ya Capripoint Mwanza. Japo kuna ukaribu wa masafa baina ya milima ya ‘Uswahilini’ ya Igogo au Bugando na milima  ya Capripoint tofauti ya hali ya mazingira na huduma iliyopo baina ya maeneo haya mawili ni kama ardhi na mbingu ama jehannamu na peponi japo kwa macho utaona kilichotenganisha milima hiyo ni sehemu ndogo tu ya maji ya Ziwa Victoria.

Kwa mfano wakati katika milima ya Igogo-Bugando ‘kibarabara’ pekee kilichopo hakiruhusu kuendesha hata baiskeli, bara bara ya milima ya Capripoint ni pana yenye lami safi, laini na isiyo na mashimo katika takriban sehemu zake zote.

Kwa upande mwengine wakati ndani ya makaazi ya milima ya Igogo hakuna hata vichochoro vinavyoruhusu kubeba jeneza kwa nafasi katika makaazi ya milima ya Capripoint kuna mitaa mipana iliyoelekea katika kila nyumba ya huko.
Vile vile wakati nyumba za Milima ya Igogo zikikosa hata mahala pa kuchimba karo za vyoo na maji machafu nyumba za milima ya Capripoint zina uwanja mpana na wenye kuruhusu kupanda bustani.


Aidha wakati kukiwa na tatizo kubwa la maji katika makaazi ya milima ya Igogo, Mahina, Mkuyuni na Nyegezi na umeme kuonekana tunu kwenye nyumba nyingi katika makaazi ya milima ya Capripoint maji ni ya ziada kiasi cha mengine kutumika kwa umwagiliaji bustani.

“Kwa vyovyote hizi ni sura zinzokinzana na hazileti picha nzuri kuwepo katika eneo linalokaribiana kama ‘mdomo na pua’ kama ilivyo milima ya Igogo na Capripoint” alisema Sanjo John nilipomtaka maoni yake baada ya kukamilisha ziara ya Milima ya Igogo na Capripoint.

Ni kwa kutembelea milima ya Capripoint tu ndipo mtu anaweza kuona ni kitu gani ambacho wakaazi wa milima ya Uswahilini (yenye makaazi holela) wanapoteza.

Jambo la kwanza ambalo ni changamoto kwa wakaazi wa milimani ni usalama wa Afya zao.Kwa kuishi katika mazingira yasiyo na vyoo vya kutosha, yasiyo na mifumo ya maji taka wala taka ngumu kama kuna jambo linalowekwa rehani hapo basi ni afya za wakaazi wa hapo na pengine wa Mwanza kwa jumla.

Afisa wa maendeleo ya Jamii mkoa wa Mwanza Isaac Ndasa aliliambia gazeti hili kuwa tatizo la mazingira duni ya wakaazi wa milima ya Mwanza haliwaathiri wao peke yao bali huwathiri pia walioko bondeni kwa vile uchafu unaozalishwa huko hauishii huko bali huishia bondeni na pengine kwenye ziwa Victoria.

Jambo la pili ambalo watu waoishi milima ya Uswahilini wanapoteza na pengine ni changamoto kubwa kwao na kwa Taifa ni thamani ya ardhi. Kwa mfano wakati Stephano John  mkaazi wa Milima ya Capripoint  akiniambia kuwa ameahidiwa  kiasi cha shilingi 200 milioni na kujengewa nyumba yenye vyumba vinne iwapo atatoa kiwanja chake kilichopo Capripoint mama Betrice hana Uhakika hata wa kupata shilingi Milioni 10 iwapo atataka kuuza nyumba yake iliopo milima ya Igogo.

Jambo la tatu ni uwezekano wa kupata huduma za mikopo ya kibenki na dhamana. Kwa mfano wakati wakaazi wa milima ya Capripoint wakiwa na uhakika wa kupata mikopo katika taasisi yoyote ya kifedha kwa kuweka dhamana ya makaazi yao yaliopo katika milima hiyo wale wa milima yenye makaazi holelela fursa ya kupata dhamana kama hiyo ni ndogo mno huko.

Jambo la nne ambalo watu wanaoishi katika makaazi holela ya milimani wanalikosa ni haki ya kuishi katika mazingira safi haki ambayo hivi karibuni ilitambuliwa na Umoja wa mataifa kuwa ni miongoni mwa haki za msingi za kibinaadamu.

Jimmy Luhende mmoja wa wanaharakati maarufu wa haki za binaadamu Mwanza nilipomuuliza kuhusu hali ya makaazi holela ya milimani alielezea hali hiyo kuwa ni ya kusikitisha. Alisema kwamba Uongozi wa jiji la Mwanza ikiwa unashindwa kulishughulikia tatizo la huko kwa umuhimu wa kuwa na mji uliopangiliwa na wenye kuvutia basi angalau na walishughulikie tatizo hilo wakijua kwamba mazingira safi  ni haki ya wananchi hao ya msingi kama binaadamu.

Wakati haiba ya milima ya Capripoint na ile ya Igogo na mingine ya Uswahilini zikikinzana kuna mkinzano pia juu ya utaratibu wa utoaji wa huduma au usimamizi unaofanywa na jiji la mwanza katika maeneo haya mawili ambayo yote kimsingi yako chini ya mamlaka yake.

Mtu anaweza kujiuliza ni jambo gani lililofanikisha uwepo wa sura nzuri katika milima ya Capripoint ambalo linashindikana kutekelezwa katika milima mengine ambayo sasa imegeuka chukizo katika sura ya mwanza. Kwa mtu ataeamua kutembelea maeneo hayo tofauti kubwa atayoweza kuigundua ni ile ya kipato kwamba wanaoishi milima ya Capripoint ni Vigogo na wenye nazo wakati wale wa milima ya Igogo na mengine ni wale ‘waliochoka’. Watu wa pwani huwaita ‘pangu pakavu tia mchuzi’

Hata hivyo tofauti hiyo haipaswi kuwa kigezo katika utoaji huduma katika nchi kama Tanzania ambayo katiba yake inatamka wazi wazi kuwa binaadamu wote ni sawa, aliniambia Kopoka Mlagiri
Nilipoulizia chanzo cha yote haya alielekeza lawama zake kwa wanasiasa kwamba wanawachochea watu ama wasihame na waendelee kukaa huko na hulitumia jambo hilo kama ajenda ya uchaguzi.

Mlagiri alisema wanasiasa hufikia kuwaambia wakaazi wa huko hasa vijana kwamba wakiwachagua hawatahamishwa huko milimani na wataendelea kuishi kama kawaida. Alisema wanasiasa kama hawa ni vigumu kupanga au kutekeleza mpango wowote wa kuwahamisha watu wa kule. “Si watakosa kura” alisema.
Mkaazi mwengine wa Mwanza, Abubakar Karsan yeye analaumu mabaraza ya Madiwani. Alisema mara zote yamekuwa dhaifu kiasi cha kushindwa kulishinikiza jiji kutekeleza wajibu wake muhimu hata kama huu wa kushughulikia makaazi holela.
Alisema tatizo  hilo ni la muda mrefu na kama ingekuwa  Baraza  la madiwani linaubana vyema uongozi wa jiji kutekeleza wajibu wake basi tatizo lingekwishamalizika zamani.

Ndoto ya Idara ya Mipango miji ya jiji la Mwanza ni kuwa na mji wenye makazi bora na usio na migogoro ya ardi lakini ni wakati tu ndio unaoweza kusema iwapo hilo litawezekana.

MWISHO