SciDev.Net

Pages

Saturday, June 2, 2012


Tanzania, Zambia zagaragazwa katika mechi za awali
Na Ali Haji Hamad
Pale kinaporoa kilemba ni muhali kwa mkuti kusalimika
Ndivyo wanavyoamini Waswahili wa Pwani. Usemi huu ulidhihirika leo katika mechi za kuwania kufuzu kucheza kumbe la Dunia huko Brazil mwaka 2014. Katika siku ambayo mabingwa wa Afrika Zambia imelala bao 2-0 mbele ya Waarabu wa Sudan kaika mechi ya kundi D, ilikuwa muhali kwa Tanzania nayo kustahimili wimbi hilo kubwa na hivyo yenyewe ikajikuta ikisalima amri mbele ya Ivory Coast kwa bao 2- 0 katika mechi ya kundi C huko Abidjan.  Ushindi huu ni mwanzo mbaya kwa timu hizi zote mbili ambazo zilionekana kupania kutaka kuvuka mabara kwenda Kusini mwa Amerika hapo 2014.

Timu nyengine zilizoanguka ni  Congo DR mbele ya Cameroon iliyochapwa 1-0 katika mechi za kundi H na Botswana mbele ya Afrika ya Kati iliyogaragazwa 2-0 kwenye mechi ya kundi A. Nyengine ni Guinea ya Ikweta iliyochapwa 3-1 na Tunisia  na Liberia iliyochakazwa kwa bao 3-1na Senegal katka mechi ya kundi J.
Sambamba na matokeo hayo kulikuwa na matokeo ya sare ya bila kufungana katika mchezo kati ya Kenya na Malawi   kundi F na Gambia na Morroco ziliotoka sare ya 1-1 katika mechi za kundi C. Bukinafaso na Congo nazo ziliishia suluhu ya 0-0 kundi E.

No comments: